Kama ndio unaingia humu kwa mara ya kwanza kabisa inawezekana kuwa unapata shida sana kuficha ujumbe katika mitandao ya kijamii hasa hasa WhatsApp. Labda una familia, marafiki au wafanya kazi wenzio ambao wana tabia ya kupekua pekua simu na kusoma meseji zako. TeknokonaDotCom inatoa msaada zaidi juu ya hili.
App hii haifanyi kazi kwa WhatsApp tuu hata facebook messenger, emails na mitandao mingine mingi inayo jihusisha na kutuma na kupokea meseji kwa haraka
APP YA KUFICHA CHAT KWENYE ANDROID
Kwanza kabisa app hii itafanya kazi katika simu za android tuu na inaitwa Messenger and Chat Lock (Chat Lock+) bofya hapa kuipakua katika simu. App ni ya bure na inapatikana katika google play store
- Pakua hiyo App kutumia Linki hapo juu au bofya hapa
- Ukishamaliza ipakua bofya kwenye Chat Lock+ kuifungua App hiyo
- Ukishaifungua, itabidi useti neno siri ambalo utalitumia katika kufungulia App
- Baada ya kuweka neno siri kuna skrini itatokea ili uchague App unazopendelea
- Chagua WhatsApp katika App hiyo ili uweze kuifunga, yaani ‘Lock’
Safi! Sasa utakapofungua WhatsApp tuu itakulazimu uingize neno siri na hili lina maanisha ‘chat’ zako zitakuwa zimefichwa kwa wale wasio jua neno siri uliloliweka. Zipo apps nyingine pia kama vile AppLock na Smart AppLock, zote zinafanya kazi ya kuzuia watu kuingia kwenye apps unazochagua, hizi tutazitathimini siku nyingine.
Kwa wale wa michepuko hata kwa wale ambao hawapendi kupekuliwa simu zao, App hii ni ya muhimu sana katika simu janja zao. App hii inasaidi kuimarisha siri katika chati mbali mbali katika simu yako.
Wazo lako ni muhimu, ningependa kusikia kutoka kwako pia tafadhali ungana nasi kupitia kurasa zetu za Facebook ,Twitter, Na Instagram
Habar natakakupata Maeleokezo kuhusu forex exchange
Unataka kujua nini kuhusu hilo?