Kampuni moja ya Korea Kusini inatengeneza saa janja (smart watch) kwaajiri ya watu wasioona ambayo itawasaidia kusoma ujumbe kutoka katika simu zao na hivyo kuwasaidia kupata taarifa ambazo walikua hawawezi kuzipata moja kwa moja.
Saa hii iliyopewa jina la DOT imetengenezwa kwa vinundu ambavyo vinauwezo wa kuhama na hivyo kuunda maandishi maalumu kwaa jili ya wasioona. saa hii inawasiliana na simu yako kwakutumia mfumo wa bluetooth na inatumia bluetooth 4.0. Kwa kutumia saa hii utaweza kusoma Messeji, barua pepe, Taarifa,na kila kitu ambacho kipo katika mfumo wa maandishi.
Vipo vifaa vingine ambavyo pia vinatumia teknolojia hii kuwasaidia watu wasioona ila tatizo ni vikubwa na pia ni ghali saana hivyo ubunifu huu wa saa janja ambayo inagharimu chini ya dola za kimarekani 300 ni suluhisho bora kwa wakati huu kwa watu wasioona.
No Comment! Be the first one.