Watafiti wanaoendesha uchunguzi katika eneo la Iceland, wanaamini kuwa wanaweza kupunguza hewa chafu inayochafua mazingira kwa kunasa hewa ya sumu ya Carbon Dioxide (CO2) na kuigeuza kuwa mawe.
Wanasayansi hao waliyeyusha hewa hiyo ndani ya maji kupuliza mchanganyiko wake ardhini, ambako ilichanganyika na madini ya Volcano na kuunda mawe yanayofanana na chokaa.
Wanasayansi hao wamesema mfumo huo unaweza kusaidia kukabiliana na mabadiliko ya viwango vya joto duniani kwa sababu mawe ya Volcano inayohitajika kugeuza gesi hiyo yanapatikana kote duniani.
Utafiti huo wa kugeuza hewa chafu kuwa jiwe ambao umechukua muda wa miaka miwili uligharimu takriban dola milioni 10. Wanapendekeza kuwa hiyo itakuwa njia thabiti ya kupambana na tabia nchi japo itagharimu pesa nyingi.
Mradi huo unaotambuliwa kama “CarbFix” unaweza kunasa hewa ya sumu kutoka angani na kuipenyeza kupitia kwenye mabomba na maji hadi ardhini. Shughuli hiyo inakamilika kwa asilimia 95% ya hewa hiyo kuganda na kuwa jiwe.
Ni wazi kuwa utafiti huu utasaidia sana maeneo ambayo yapo karibu na viwanda hivyo kufanya watu kuepuka kuvuta harufu mbaya kutoka viwandani na kuwafanya watu kuugua magonjwa mbalimbali kutokana na kuvuta hewa zenye kemikali na kiwango kikubwa cha CO2.
Teknolojia hiyo… endelea kutembelea TeknoKona na tutaendelea kukuletea habari kuhusu maendeleo ya teknolojia hii.
Vyanzo: https://www.or.is/english/carbfix-project na mitandao mbalimbali