Space X wamekwisha fanya safari kadhaa za roketi na kufanikiwa kuzishusha roketi hizi duniani ili zitumike tena. Jana walirusha tena roketi nyingine lakini safari hii hawakufanikiwa kuirudisha salama ardhini.
Space X safari hii walikuwa wanarusha satelite mbili za mawasiliano za Eutelsat na ABS, baada ya kuzifikisha roketi hizo katika obit yake roketi hiyo ilirudi duniani ila wakati wa kutua katika meli maalumu ilianguka.
Space X walikwisha fanya safari kama hii na kufanikiwa kurudisha roketi katika hali ya usalama mwezi Mei, Kwa mujibu wa CNN tukio hili lilitegemewa kuwa gumu kidogo kutokana na ukweli kwamba roketi hiyo ilikuwa inaenda anga la mbali hivyo ingerudi na mwendo mkali zaidi.
Kila kitu kilikuwa kinaonekana kinaenda sawa mpaka pale ambapo matangazo ya moja kwa moja yalipokatika sekunde chache kabla ya roeketi hiyo kutua katika meli maalumu na kuwaacha waliokuwa wakifuatilia tukio hilo bila ya kujua nini hasa kimetokea.