Toleo jipya la gemu la Fifa, Fifa 17 kuja hivi karibuni. Kila mwaka toleo jipya la video game ijulikanayo kama “Fifa” inatoka. Makala hii inakuelezea kuhusu toleo jipya la FIFA 17 kutoka “Electronic Arts (EA)” .
>Utaweza kukuza kipaji cha mchezaji mmoja ndani na nje ya uwanja
Toleo lililopita (Fifa 16) lilifanya vizuri katika soko la mauzo katika Play Station na Xbox. Fifa 16 ni moja video games zinazopendwa zaidi pamoja na video games zingine kama vile Star Wars: Battlefront.
Katika utangulizi gemu hili linachaguo la kucheza katika mfumo wa hadithi (story) ambao umeitwa “The journey” (safari) ikiwa ni hadithi (story) kuhusu mchezaji mpira aitwaye Alex Hunter.
Katika video fupi(trailer) iliyooneshwa kwenye “EA Event” ilimuonesha mhusika (Alex Hunter) akiwa na familia yake, meneja wake akimfuata kwa ajili ya mazungumzo nae, akigombana pia katika trailer hiyo ilimuonyesha mhusika akigombana na mchezaji mwenzake.
Katika trailer hiyo Hunter alionekana akiichezea Manchester United lakini EA walisema kuwa mchezaji kutakuwa na uwezo wa mchezaji gemu hilo (gamer) kumtumia mchezaji huyo katka vilabu vingine katka ligi kuu ya Uingereza kulingana na si kumtumia akiichezea Man U pekee.
>Vitu vinginevyo vilivyomo katika Fifa 17
- Uwezo wa kutumia “Frostbite games engine” ambayo itawezesha muonekano wa picha (graphics) kuwa hali ya juu
- Kujumuishwa kwa makocha wanne: Jose Mourinho, Pep Guardiola, Arsene Wenger na Jurgen Klopp katika timu ambazo ni kali na zenye mvutio
- Mbinu mpya za kufanya mashambulizi ambazo zitamuongezea gamer uwezekano wa kufunga mabao.