Ni vigumu kuongelea mabingwa katika utengenezaji wa simu janja zinazofanya vizuri sana sokoni bila kuwataja Samsung. Ila unafahamu ya kwamba safari katika biashara ya simu ilianzia wapi? Leo fahamu mwanzo wao.
Samsung ni kampuni yenye biashara nyingi sana zaidi tu ya simu, na ingawa Samsung ipo tokea mwaka ni mwaka 1985 ndio walitengeneza simu yao ya kwanza kabisa.
Simu hiyo ilikuwa ni Samsung SC-1000 na ilikuwa ni simu inayokaa kwenye magari. Haikufanya vizuri, na matokeo yake Samsung waliwekeza miaka miwili katika utafiti zaidi.
Na wakaja na simu iliyoitwa Samsung SH-100, iliyoingia sokoni mwaka 1988. Hii ndio simu ya mkononi ya kwanza kabisa kutoka Samsung.
Pia simu ya Samsung SH-100 ndiyo ikawa ndio simu ya mkononi ya kwanza kabisa kubuniwa na kutengenezwa nchini Korea ya Kusini.
Wakati huu, 1988, kampuni nyingine kama vile Nokia walikuwa washaingiza sokoni simu za mkononi za aina tatu tuu – hii inakupa picha ya maendeleo makubwa yaliyofikiwa na Samsung kwa kipindi hicho.