Mitandao maarufu ya kijamii yenye watumiaji wengi Facebook na Snapchat sasa kuweza kutuma na kupokea pesa au kufanya malipo kwa kutumia mitandao hiyo ya kijamii.
Nchini Marekani watumiaji wa Facebook wanaweza kutuma pesa bila gharama yoyote kwa mtu kwa kutumia Facebook Messenger. Utumaji huo wa pesa pia umwezesha mtumiaji kuweza kufanya malipo ya kitu fulani kama vile kfanya malipo katika mgahawa, n.k.
Pia watumiaji wa Snapchat wanaweza kutuma pesa kwa kutumia app ijulikanayo kama “Snapcash“. App hiyo imeundwa kuweza kurahisisha malipo kwa haraka na urahisi zaidi ambapo mtu anaweza kulipia tiketi ili kuweza kuingia kwenye tamasha, kulipa kwenye mgahawa, n.k.
Teknolojia hiyo ya kulipa kwa kutumia FB Messenger na Snapcash inatarajiwa kuingia nchini Uingereza hivi karibuni hivyo kuwezesha nao kuweza kufanya malipo kwa kutumia apps hizo.
Jinsi ya kufanya malipo katika mitandao hiyo
Ili mtu aweze kufanya malipo kwa kutumia mojawapo ya applications hizo ni lazima awe na miaka 18 au zaidi. Pia awe na “Debit card”. Mtu hawezi kufanya malipo kwa kututmia “Credit cards/Paypal akaunti” kwa sababu hazikubaliki.
Ili kuweza kulipia kwa kupitia FB Messenger unachotakiwa kufanya ni kufungua chat kisha unabonyeza “More” kisha unabonyeza “$” ma kisha kubofya neno “Pay“(lipa). Kwenye Snapcash unachotakiwa kufanya ni kufungua chat kisha unabofya “Add card” ili kuweza kuweka namba za debit card inayotumika Marekani.
Kutokana na huduma hii ya kufanya malipo kwa kutumia apps hizo inapatikana Marekani tu kwa sasa basi mtu yeyoyote amabaye anataka afanye malipo kwa kutumia njia hii inabidi awe Marekani na sio nje ya hapo kwa sababu kwingineko huduma hiyo bado haijafika.
Imeelezwa kuwa malipo hayo kwa njia ya mtandao wa kijamii yapo salama na si rahisi kudukuliwa na mtu kuibiwa pesa zake. Je, una maoni gani kama teknolojia hii ikija kwetu Afrika? Endelea kufuatilia habari kadha wa kadha kupitia Teknokona
Chanzo: The Telegraph, CNET