Makampuni mbalimbali yamefunga hesabu za robo ya pili ya mwaka ambapo pamoja na yote yameangalia faida ama hasara iliyopatikana.
Twitter kwa upande wao mambo sio mazuri baada ya kushindwa kufikia malengo ambayo walijiwekea hata hivyo wenyewe wameonesha kuchukua mtazamo chanya na kuwa na matumani.
Kushindwa kufikia hesabu huku kwa Twitter kunawafanya kwa sasa kuwa na hali mbaya ya kibiashara kwakuwa bei ya hisa zake inazidi kushuka.
Hizi ni baadhi ya takwimu ambazo zimetolewa pamoja na ripoti hiyo:-
- Kwa sasa watumiaji walio hai wa mtandao huu wamefikia milioni 313 kutoka milioni 310 katika robo ya kwanza ya mwaka, hii bado ni nyuma sana ya mitandao ambayo inafanya vizuri kama vile Facebook ambao umefikisha watumiaji bilioni moja.
- Mapato ya Twitter pia yamekuwa mpaka dola za kimarekani milioni 602 ingawa haya pia ni bado chini ya malengo.
- Hasara katika robo hii ya mwaka imezidi kupungua kutoka dola milioni 136 mwaka jana hadi dola milioni 107
Hii inamaana gani kwa Twitter?
Jack Dorsey ambaye ndiye mkurugenzi mtendaji anasema kwamba wamepiga hatua katika kushughurikia vipaumbele katika robo hii ya mwaka na kwamba wanaimani na mipango waliyojiwekea.
Hii inaonesha kwamba mabadilko mbalimbali kama vile kuleta algorithmic timeline yanaaanza kuzaa matunda na hivyo mabadiliko yataendelea.
Ni wazi kwamba waliozani kwamba kwa kufanya mabadiliko Twitter itakufa wako katika upande unaopoteza.
Endelea kusoma makala zetu nyingine na kutushirikisha maoni yako katika sehemu ya maoni nasi tutajibu