Mashindano ya Olimpiki mwaka huu yanafanyika nchini Brazil na tayari yamekwisha kamata vichwa vya habari vya mitandao mingi ya habari baada ya kutokea sintofahamu hasa baada ya washiriki kutoka Urusi kutaka kuzuiwa kushiriki katika michezo hii kwakushutumiwa kutumia dawa za kuongeza nguvu.
Mashindano haya yapo katika hatua za mwisho za maandalizi na yanatarajiwa kuanza ijumaa hii, Twitter wanaonekana wapotayari kukamata fursa juu ya mashindano haya kwa kwa kuwa tayari wamekwisha toa seti ya emoji kwa ajiri ya kuhamasisha watu kujihusisha na habari za mashindano haya katika mtandao huu.
Hii sio mara ya kwanza kwa Twitter kukamata fursa katika michezo!
Tayari tulikwisha kuona mashindano ya kombe la ulaya yaliongelewa sana katika mtandao huu na hivyo kusaidia kupata mapato kutokana na matangazo, sasa Twitter inataka kukamata fursa tena huko Brazil katika Olimpiki kwa kuhakikisha kwamba watu wanaiongelea zaidi michezo hiyo katika mtandao huu.
Twitter imetoa emoji kwa kila nchi ambayo inashiriki katika mashindano haya ( hata Tanzania imo na pia inayo emoji yake ambayo utaipata kwa kuandika #TAN ) pamoja na kuwa kila nchi ina emoji yake ambayo kimsingi ni emoji ya bendera ya nchi husika bado kuna emoji nyingi kwaajiri ya kila mchezo ambao utashindaniwa huko Brazil na pia kutakuwa na emoji za zawadi ama medali.
Pamoja na emoji hizi Twitter pia watatengeneza channel maalumu kwaajiri ya kurusha habari za mashindano haya katika app zake za Periscope pamoja na Vine. Kwa kifupi ni kwamba kwa kuwa Twitter basi mtumiaji hataweza kupitwa na mashindano haya, hii ni habari nzuri kwa wenzangu na mimi ambao ni washabiki wa michezo kupitia TL.
Teknokona inaendelea kufuatilia mashindano haya kwa karibu na kama kuna lolote upande wa teknolojia basi sisi ndio tutakuwa wa kwanza kukuletea taarifa hiyo. Kaanasi.