Tarehe 6 mwezi wa nane miaka 25 iliyopita website ya kwanza duniani ilianza kuwa hewani kwa mara ya kwanza.
Tovuti ya kwanza kwenda hewani ilionekana kwa mara ya kwanza Agosti 6 1991 ambayo ilikuwa ikielezea undani wa project ya wakati huo iliyoitwa WWW(Wide World Web) na kueleza jinsi ambavyo mtu anaweza akatengeneza web server yake mwenyewe, kuweza kutengeneza tovuti na kurasa zao wenyewe.
Tovuti hiyo ilijulikana kama http://info.cern.ch/hypertext/WWW/TheProject.html (haipo hewani tena) ambayo pia ilieleza jinsi ambavyo mtu anaweza kutafuta kitu kwenye tovuti.
Kwa tafsiri isiyo rasmi WWW ni kiunganishi kinachowezesha kukupeleka kwenye tovuti husika popote utakapokuwa duniani.
Hapo awali ilikuwa ni lazima kutanguliza ‘WWW’ kabla ya tovuti husika ingawa kwa hivi sasa si lazima kuanza na WWW.