Watu ambao wanatumia wireless keyboard kwenye kompyuta kuna uwezekano wa nywila, na taarifa zako nyingine unazoandika kujulikana.
Watu ambao wanatumia Wireless keyboard za bei rahisi wana hatari ya username na passwords zao kudukuliwa kitendo ambacho kinaweza kusababisha taarifa zao kuonekana kwa watu ambao haziwahusu.
Imeelezwa kuwa aina 8 za wireless keyboards zinazopendwa kutumika duani kote zinaweza kudukuliwa hata katika umbali wa mita 100 na kumuwezesha mdukuzi kujua kile unachokiandika kupitia kompyuta au kifaa kingine chochote ambacho unaweza kuandika kwa kutumia keyboard.
Mbinu ya udukuzi uliyoitwa KeySniffer ilimuwezesha hacker kuweza kupata taarifa muhimu za kadi ya benki madhalani, username, nyilwa, majibu ya security questions kwa ajili ya email address pamoja na nyaraka nyingine muhimu.
Tafiti zinaonyesha kuwa aina mbalimmbali zilifanyiwa majaribio na 8 kati ya hizo zilionyesha uwezekano wa kudukuliwa kutoka makampuni ya Toshiba na HP ambazo hazitumii bluetooth kuunganishwa na kompyuta bali kutumia masafa ya wazi ya radio(un-encrypted radio signals).
Jinsi udukuzi huo ulivyofanikiwa
Kilitumika kifaa ambacho kilivuruga mawasiliano kati ya keyboard na blutooth receiver. Mbali na keyboard zinatumia bluetooth kuunganishwa na kompyuta hakuna aina nyingine ya bluetooth iliyo salama katika suala zima la udukuzi.
Jinsi ya kuepuka kudukuliwa kupitia Wireless keyboard
Hakuna njia rahisi ya kuepuka tatizo ila unashauriwa kuwasiliana na kampuni iliyotengeneza keyboard hiyo na ili waweze kukupa kifaa ambacho ni nadubuti zaidi na kukufanya maboresho ya kila mara ili kuepuka usumbufu.
Ni vizuri kukunua kifaa (wireless device) ambacho kina maelezo ya kina kuhusu kifaa hicho na kama haukiamini kabisa. TeknoKona imakushauri kukunua ambacho sio wireless bali kilichounganishwa na waya(wired device).
Chanzo: The Telegraph