Mbwa wawili ambao wamepewa mafunzo ya jinsi ya kunusa meno ya tembo wameanza kazi katika hifadhi ya Ruaha na tayari wamekwishafanikiwa kukamata nyara kwa mara ya kwanza.
Kwa mujibu wa shirika la Wild Life Conservation Society Dexter na Jenny walifanikiwa kusaidia askari wanyama pori wa hifadhi ya Ruaha kukamata pembe za ndovu mchanga ambazo katika msako wa kawaida askari hao hawakufanikiwa kukamata pembe hizo.
Mbwa hao walipoletwa walifanikiwa kuipata harufu iliyowapeleka katika uvungu wa gari nje ya nyumba ambako kulikuwa na pembe hizo.
Hii ni mara ya kwanza kwa wanyama hao wawili ambao kusaidia kukamata nyara tangu walipoletwa nchini kukabiliana na tatizo la ujangili. Kumekuwa na ongezeko wa shughuri za kijangiri katika hifadhi na mbuga za wanyama nchini jambo ambalo limesababisha upungufu wa tembo.
Shirika la WCS limekuwa likifanya kazi kwa karibu na mamlaka za hifadhi za wanyamapori Tanzania, jitihada ambazo zilisaidia Mbwa hawa kupewa mafunzo na kampuni ya huko Uingereza.
Mbwa hao watasaidia kupunguza Ujangiri katika hifadhi ya ruaha lakini pia mafanikio yake katika mbuga hii yanaweza kuwa chachu ya aina hii ya ulinzi kutumika katika mbuga nyingine.
Taarifa hii imeripotiwa na jarida la Huffington Post