Kampuni ya Samsung ipo njiani kupata hasara kubwa kutokana na makosa makubwa katika betri za Samsung Galaxy Note 7 ambapo sasa inawabidi kuondoa simu hizo duniani kote.
Data zinaonesha katika kila simu milioni 1 za Samsung Galaxy Note 7 kuna simu 24 ambazo betri zake zina hatari ya kulipuka. Mpaka sasa kuna simu 35 ambazo taarifa za uhakika
Samsung wamesema wameingiza takribani simu milioni 2.5 za Galaxy Note 7 kwenye soko (madukani, na nyingine tayari zimenunuliwa). Simu za Galaxy Note 7 zilianza patikana tena rasmi kuanzia mwezi wa nane mwaka huu.
Familia za simu za Galaxy ndio zinaongeza kwa kuingizia mapato kampuni ya Samsung na inategemewa hatua hii ya wao kurudisha simu zote hizo na kuzihakiki kutawasababishia hasara kubwa sana.
Samsung imesitisha usafirishaji wa simu hizo kwa kampuni tatu kuu zinazosafirisha simu hizo hadi maeneo mbalimbali duniani ili kufanya uchunguzi zaidi na mpaka sasa imeshapokea kesi 35 kuhusiana na betri za simu hiyo kuwa na matatizo.
Mtu mmoja katika YouTube anaishi Marekani, aliweka mtandaoni video inayoonesha Galaxy Note 7 ikiwa imeungua na skrini yake kuharibika na kusema kuwa simu yake ilishika moto baada yake kuitoa kutoka kwenye chaja rasmi ya Samsung, chini ya wiki mbili.
Bw. Koh Dong-jin ambaye ni rais wa Samsung amesema kuwa ni kweli betri za simu hiyo mpya sokoni zina tatizo ambalo ilikuwa ni vigumu kulitambua wakati wa utengezwaji wa betri hizo. Lakini pia amekataa kumtaja msambazaji wa betri zenye matatizo. Aliongeza na kusema kuwa Samsung walikuwa na makubaliano na wasambazaji watatu akiwemo Samsung SDI waliochini ya Samsung wenywe.
Simu zote zinazorudi kwao bado hawajasema nini kitafanyika wakishabadilisha betri zake, ila wengi wanaona zinaweza husika katika utaratibu wao mpya wanaotaka kuuanzisha wa kuuza simu zilizofanyiwa marekebisho/kutumika kwa bei nafuu.
Hii changamoto imekuwa inagusa zaidi makampuni ya magari mara kwa mara, ila pia ata Nokia mwaka 2007 iliwabidi kurudisha kiwandani simu zaidi ya milioni 46 baada ya kesi ya simu 100 kuwa na joto kali sana linaloweza sababisha mlipuko.
Vyanzo: The guardian, BBC