Watumiaji wa moja ya tovuti/mtandao mkubwa wa video za ngono duniani, Brazzers.com wiki hii watakuwa katika hali ngumu kisaikolojia baada ya data za kuwahusu kuwekwa wazi na wadukuzi.
Data hizo zinawahusu takribani watumiaji 800,000 wa tovuti hiyo na data zinajumuhisha majina ya watumiaji hao na taarifa zao zingine kuhusu wapendavyo ndani ya tovuti kubwa hiyo ya ngono.
Inasemekana udukuzi wa data hizo ulifanyika mwaka 2013 ila ni sasa ndio wadukuzi hao wamehamua kuweka wazi data za watumiaji wa tovuti hiyo.
Udukuzi wa kuingilia mifumo yote ya data ulifanyika baada ya kufanikiwa kudukua eneo la mazungumzo (forums) la tovuti hiyo. Wadukuzi waliweza kuingilia njia hiyo kutokana na wasimamiaji wa tovuti ya Brazzers kutosasisha mfumo mzima unaotumika kutolea huduma za forums – unafahamika kwa jina la vBulletin.
Katika swali ambalo TeknoKona imeuliza watembeleaji wake kwa zaidi ya miezi 15 inaonekana ata Tanzania utumiaji bado upo juu. Zaidi ya asilimia 70 kati ya watu zaidi ya 200 walioshiriki kujibu walisema washawahi au bado wanatembelea mitandao ya ngono.
[socialpoll id=”2256886″]