Kutokana na tetemeko la ardhi lililoikumba baadhi ya maeneo nchini Tanzania imezua maswali mengi na mojawapo likiwa kama kuna uwezekano wa kuweza kubashiri ujio wa tetemeko la ardhi kabla ya kutokea.
Ni hivi majuzi tu Tanzania maeneo ya Kask. Magharibi mwa nchi hiyo imekumbwa na tetemeko la ardhi tukio lililosababisha huzuni kubwa kwa wananchi wa maeneo husika na nchi nzima kwa ujumla. Ni tukio lililosababisha uharibifu wa makazi ya watu na vifo takribani vya watu 16 mpaka sasa.
Kwa mujibu wa BBC ilipofanya mahojiano na Prof. Fulbert Namwamba aliweza kueleza uwezekano wa kubashiri tetemeko la ardhi. Watafiti nchini Uchina wanasema wakati fulani unapoona wanyama kama mbwa wakibweka sana isivyo kawaida pamoja na ndege wakitoa sauti zao kwa juu sana basi ni ishara ya tetemeko la ardhi kuweza kutokea katika siku za usoni.
Watafiti hao walienda mbali na hata kuthubutu kuweka kioo kikubwa sehemu ya wazi na kama kioo hicho kikivunjika katika siku za usoni basi ni ishara tosha kuwa tetemeko la ardhi litatokea katika siku za usoni.
Kwa kawaida tetemeko hutokea kila baada ya miaka mamia hata hivyo watu wanaoishi na maeneo karibu na bonde la ufa wanashauriwa kujenga nyumba zilizo imara/kama ni nyumba ina ya ghorofa basi ni muhimu kuhakikisha wanatumia nondo zilizo imara barabara.
TeknoKona inatoa pole kwa watu wote waliokutwa na maafa haya yasiyo na wa kumlaumu. Daima tushikamane katika raha na shida.
Vyanzo: BBC, Prof. Fulbert Namwamba