Inawezekana mwaka huu usiwe mwaka mzuri kwa Apple kwani imekuwa ikikabiliana kwa kulipa faini kwa makampuni mbalimbali kutokana na kuwa na hatia.
Apple ni kampuni nguli katika masuala ya teknolojia lakini kwa kuendelea kukutwa na hatia kwa kosa la kuiba hatia miliki inaishushia hadhi kampuni hiyo. Kwa mara nyingine tena Apple imeamriwa kuilipa kampuni ya VirnetX Holding Corp takribani dola 302.4 milioni|zaidi ya Tsh. bil 660.
Hukumu hiyo imetokana na moja ya features (FaceTime) iliyopo kwenye simu za familia ya iPhones ambayo ina hati miliki inayomilikiwa na VirnetX Holding Corp.
Virnetx ni kampuni ya mawasiliano ilianzishwa na wafanyakazi wa Science Applications International Corp. (SAIC) ambayo ilitengeneza teknolojia ya ulinzi kwa taasisi mbalimbali za usalama.
Hii ni mara ya tatu kwa Apple na Virnetx kuingia katika sakata la hati miliki ambapo mwaka 2010 Apple iliamriwa kuilipa $368.2 milioni ambayo ni sawa na zaidi ya Tsh bil. 804 lakini mahaka ilitupia mali rufani hiyo. Rufani ya pili ilitoka Mwezi Julai Virnetx imeshinda na Apple waliamualiwa kulipa dola 625.6 milioni|zaidi ya Tsh 1,336 bil.
Siku zote Apple huwa hawakubali kushindwa na kwa mara nyingine wanatarajiwa kukata rufaa kuhusiana na kesi inayowakabiliana sasa hivi. Kama watashindwa rufani itawazalimu kulipa zaidi ya Tsh bil. 660.
Vyanzo: The verge, engadget