Uwepo wa shule unaweza usiwe na maana kwa kiasi kikubwa iwapo watoto wakiruhusiwa kujifunza online.
Mwezi uliopita serikali ya New Zealand ilipitisha mswada wa sheria utakaomruhusu mtoto wa umri yoyote kuweza kujifunza masomo yake mtandaoni (online).
Mswada huo pia utakuwa na jukumu la kuamua iwapo mwanafunzi atakuwa na umuhimu wa kuwepo shule ana kwa ana au awe anakwenda shule kwa siku chache tu katika wiki.
Katika hali ya kustaajabisha mabadiliko hayo ya sheria yamepokelewa vyema na umoja wa walimu wanaofundisha shule za msingi ingawa wachambuzi wa masuala ya elimu wamekosoa mabadiliko hayo na kuuliza kama uwepo wa shule utakuwa na umuhimu.
Mafunzo ya mtandaoni yanatoa wigo mpana kwa mwanafunzi kuweza kusoma masomo mbalimbali ambayo kwa namna moja au nyingine asingeweza kuyapata akiwa shuleni. Pia kusoma mtandaoni ni muhimu kwa yule ambaye alikuwa hana uwezo wa kujiunga na shuke/chuo kutokana na kipato kidogo au kuwa mgonjwa.
Ukuaji wa teknolojia hasa intaneti duniani kote ndio umewezesha masuala kama haya kuzaliwa kwani mambo masuala ya kusoma online si jambo geni kwa nchi nyingi Afrika lakini kikubwa cha kujiuliza ni walimu katika shule zetu wataendelea kuwa na ajira zao? Tupe maoni yako tafadhali.
Kumbuka kusambaza makala na pia kuungana nasi kupitia Facebook, Twitter, Instagram, YouTube, Telegram na Google Plus
Vyanzo: telegraph.co.uk, mitandao mbalimbali