Twitter inaweza ikapunguza wafanyakazi wake kwa kiasi kikubwa sana, wafanya kazi wa ndani ambao wanaijua taarifa hiyo wamedokeza kuwa inawezekana kazi 300 zikapunguzwa.
Nguvu kazi ya Twitter inaweza ikaathirika kwa asilimia 8 kama hili likitokea. Unaweza ukajiuliza ni kwanini haya yote yanatokea lakini ukweli ni kwamba kampuni linafanya vibaya siku hizi katika maswala mazima ya kifedha.
Licha ya fedha tuu twitter vile vile imeshindwa kujipanua na kuongeza watumiaji wengi zaidi na pia taarifa zingine zilizotoka kwamba kampuni hilo linataka kujiuza lakini mpaka sasa hajajitokeza mnunuzi.
Mmiliki wa Twitter pia anamiliki makampuni mengine yanayojitegemea na hili limewafanya watu kuanza kujiuliza maswali kama ni kweli anaweza kuendesha makampuni yote hayo na kuhakikisha kuwa anapata matokeo chanya (twitter iko mbioni kumshinda).
Kumbuka watu wote ambao hapo mwanzo waliweka nia ya kuinunua kampuni ya twitter (Salesforce, Alphabet, Walt Disney) wote walijitoa katika mchakato huo.
Kama kazi hizi zilikuwa hazina umuhimu mkubwa kuzipunguza ni jambo zuri. Ukiachana na hilo pia kama kazi nyingi zinaweza zikafanywa na mtu mmoja basi ni vizuri pia. Hii itawasaidia Twitter hata kukusanya faida kubwa kidogo ukilinganisha na mwanzo.