Katika hali inayoonesha mtandao wa kijamii maarufu unataka kushindana moja kwa moja na LinkedIn, mtandao maarufu wa masuala ya ajira na urafiki wa kikazi na kibiashara.
Mabadiliko ambayo yapo njiani kwenye mtandao huo wa Facebook yatazipa Pages (Kurasa) za kibiashara na makampuni uwezo wa ku’post nafasi za Ajira kwenye kurasa zao.
Kuna uwezekano Facebook ata wakatoza makampuni pesa ili nafasi hizo za ajira zionekano kwa watu wengi zaidi.
Nafisi hizo za ajira zitaweza kuonekana kupitia eneo la pembeni kwenye page hizo maarufu kwa jina la ‘Tabs’. Hili ni eneo linalokupa uwezo wa kwenda moja kwa moja kwa vitu kama vile Video, Picha, na taarifa zingine zilizopo kwenye ukurasa husika wa Facebook. Kuelewa zaidi angalia picha hii;
Mtandao wa LinkedIn ambao tayari una umaarufu mkubwa katika eneo la mahusiano ya kiajira na utafutaji nafasi za kazi bado upo sehemu nzuri sana na inawezekana kwa kiasi kikubwa hawataathirika na maboresho haya kutoka Facebook.
LinkedIn pia umenunuliwa hivi karibuni na Microsoft, hivyo kuna uwekezaji mkubwa unaendelea na wapo katika eneo zuri kiushindani kiasi ya kutoathirika na ujio wa maboresho haya kutoka Facebook.