Wateja zaidi ya laki moja wakosa intaneti baada ya makampuni yanayotoa huduma ya intaneti kushambuliwa na kirusi kiitwacho Mirai. Kiasi hicho cha udukuzi kimeingia katika kumbukumbu kutokana na kuathiri kompyuta nyingi sana.
Uharibifu huo ullizikumba kampuni kubwa kama Talk Talk, shirika la Posta la Uingereza na KCom. Udukuzi huo ulisambazwa na kompyuta ambazo zilikuwa zimeathiriwa na kirusi Mirai.
Takwimu zinaonyesha karibu wateja 100,000 wa shirika la Posta la Uingereza walipata ugumu katika shughuli zao, KCom-zaidi ya wateja wake 10,000 waliathiriwa na uvamizi huo wa kimtandao huku Talk Talk wakikubali kuwa kirusi hicho kimeathiri lakini wakakataa kutoa idadi ya wateja wake waliothiriwa na uharibifu uliofanywa na kirusi Mirai.
Si Uingereza tu ndio ilikuwa imeathiriwa na kirusi hicho siku chache kabla ya Uinereza kuvamiwa kimtandao na kirusi hicho kampuni moja ya mawasiliano nchini Ujerumani ilisema wateja wake zaidi ya 900,000 walikosa huduma ya intaneti kwa kisa kinachofanana na Uingereza.
Hakuna mtu/kundi la watu waliosema wanahusika na udukuzi uuliofanyika nchini Ujerumani ingawa kundi la udukuzi kutoka Urusi linashukiwa kuhusika na uhalifu huo.
Hatua madhubuti zimechukuliwa na makampuni husika kwa kuwziongezea routers usalama zaidi ili zisiweze kuathiriwa na wadukukuzi.
Vyanzo: The guardian, mitandao mbalimbali.