Samsung inaweza ikawa ni simu janja pekee ambayo haijawahi kutoa simu zenye kamera mbili za nyuma kama simu janja nyingine kama zile za Tecno na Huawei.
Lakini hili linaweza likazimwa hivi karibuni tuu maana inasemekana kuwa kampuni hiyo iko mbioni katika kutoa toleo la simu ambayo inasemekana kuwa itakuja na kamera mbili za nyuma
Simu hiyo inajulikana Samsung Galaxy J7 ambayo inasemekana ambayo itakuja na kamera mbili za nyuma
Kamera mbili siku hizi imekua kama ni kitu ambacho simu mpya zinazokuja inakiangalia kwa jicho la tatu.
Swala hili limekuja kupata kiulizo baada ya kampuni moja huko china kuweka picha za makava magumu ya simu ya Samsung Galaxy J7 ambazo zilikuwa zina matobo ya kamera mbuli kwa nyuma.
PENGINE HII INAWEZA ISIWE YA KWANZA!
Ndio kabisa pengine hii inaweza ikawa sio ya kwanza ambayo itakuja na kamera mbili kwani kumbuka kabisa hapo awali ilisemekana kuwa simu ya Samsung Galaxy NOTE 8 ilisemekana kuw ainaweza ikatoka na kamera mbili pia
Licha ya simu hiyo bado simu ijulikanayo kama Samsung Galaxy C10 nayo ilisemekana kuwa inaweza ikaja na kamera mbili.
Kwa taarifa hizi za haraka haraka ni vigumu kujua kwa kina kuwa ni simu ipi kati ya hizi itakuwa ni ya kwanza kutoka na kuandika historia kuwa ya kwanza kuwa na kamera mbili za nyuma.
Pia ukifikiria sana unaweza ukagundua kitu kuwa simu za Galaxy C10 na Galaxy J7 zinaweza zisije na kamera mbili hata hivyo kwa kuwa hazina ukubwa kama ile ya Note 8. Pengine NOTE 8 ndio inaweza ikaja na mbwembwe za kamera mbili