Kampuni ya simu maarufu ya Tecno iliingia ubia na Klabu kubwa duniani ya Manchester City mwaka 2016. Katika ushirika huo inasemekana makampuni yote mawili yamekaa chini na kufikia muafaka wa kutoa simu janja ambayo itakua na chapa za makampuni yote mawili.
Ni jambo zuri sana kwani Tecno moja kwa moja wataweza kuwafikia mashabiki wa dhati wa Man City kwa kuwapa kile ambacho wamekitegemea kwa muda mrefu na pia hata wale wateja wao wa kila siku watapata kitu kipya.
Kujua Ubia Huo Zaidi Ingia Hapa
Lengo ni kuleta bidhaa ambazo zitakuwa na uhusiano wa moja kwa moja na klabu hiyo. Bidhaa ambayo itatumika si nyingine bali ni simu kutoka Tecno ya toleo la Camon CX.
Toleo la Camon CX ni moja kati ya matoleo ya simu za Camon kutoka Tecno. Sifa kubwa katika simu janja hizi ni kwamba huwa zinakuja na kamera kali zaidi.
Kwa haraka haraka taarifa zilizopo ni kwamba simu itakuja na kamera yenye MP 16. Kamera ya mbele itakua na flashi mbili. Teknolojia ya alama za vidole itakuwepo ambayo itaweza kuhakikisha kuna usalama wa juu katika kifaa chako.
Inasemekana mtu atakuwa na uwezo wa kupiga picha kwa haraka/kasi zaidi yaani kwa kutumia sekunde 0.1 tuu
Muonekano wake utakuwa ni wa kijanja zaidi na ukiwa ndani ya simu utaweza kutumia angalau App 50 bila ya simu kugandaganda (Stuck) kwani ina RAM ya GB 4.
Sifa zingine za undani tutakujuza kwa kina katika siku za usoni.
Katika upande wa bei hatuna tatizo na Tecno, japokua hatujaijua lakini tunachojua ni kwamba simu za Tecno huwa zinakuja na hadhi kubwa na kuuzwa kwa bei ndogo