Wiki hii kampuni ya mtandao wa simu ya Airtel Tanzania, imezindua ofa mpya inayokwenda kwa jina la HATUPIMI Bando. Haya ni ya kufahamu kuhusu bando hilo.
Kwa wateja wa Airtel habari hii inaweza ikawa ni moja ya habari njema kwao.
- Bando hili litapatikana katika vifurushi vya siku, wiki na mwezi.
- Sifa kubwa ni kuwapa uwezo wateja wa Airtel wanaopiga simu kwenda wateja wengine wa Airtel kuongea bila ya kupimiwa dakika za maongezi.
- Virushi vipo kwa bei mbalimbali, mfano kuna cha siku kwa Tsh 1,000/=, pia kuna cha wiki kwa Tsh 5,000/= na pia kuna cha mwezi kwa Tsh 10,000/=
- Vifurushi vyote pia vinakuja na dakika za maongezi kupiga mitandao mengine yote.