Tayari mialiko imeshatunwa kwa watu mbalimbali ili kuja kuhudhuria uzinduzi ambao unatarajiwa kuwa wa kipekee sana kutokana na sehemu utakapofanyikia uzinduzi huo na hata soko la bidhaa zenyewe.
Apple ambao wanajulikana kwa kufanya uzinduzi katika kumbi mbalimbali na hata kudiriki kujenga ukumbi wao wenyewe kwa ajili ya shughuli mbalimbali lakini Machi 27 mwaka huu (2018) wanatarajia kuzindua bidhaa zao kitofauti.
Je, uzinduzi huo utakuwa wa kitofauti kivipi?
Apple watafanya uzinduzi huo katika shule moja ya sekondari iliyopo Chicago, Marekani na sababu ya kuamua kufanya uzinduzi kwenye shule ya sekondari ni dhima ya tukio zima; uzinduzi wa bidhaa zinatazolenga sekta ya elimu na kuonyesha teknolojia mpya zinaweza kutumiwa na walimu pamoja na wanafunzi.
Mara ya mwisho Apple kufanya uzinduzi kwenye shule ya sekondari ilikuwa mwaka 2012 jijini New York.
Vinavyotarajiwa kuzinduliwa Machi 27.
Mbali na kuwa Apple watazindua vifaa vya kiteknolojia vitakavyolenga sekta ya elimu zaidi mathalani iPad ya inchi 9.7 mahususi kwa ajili ya elimu itakayokuwa inauzwa $259 na kutokuwa na teknolojia ya FaceID; iPad zitakazokuwa na teknolojia ya hali ya juu ya kamera, Animoji na ARKit zinatarajiwa kutoka baadae mwaka huu.
Inasemekana katika uzinduzi huo wanatarajia kutambulisha toleo jipya la MacBoook Air ambayo ni miaka sasa imepita bila toleo jipya la kompyuta hiyo kutoka; hata bei yake inaweza kuwa kati ya $799-$899|zaidi ya Tsh. 1.8M-2,025M ili kuwezesha watoto wa sekondari na vijana walio vyuoni kuweza kununua.
Kubwa zaidi Apple wanatarajiwa kutumia teknolojia ya AR (Augmented Reality) kuwapeleka watoto kwenye safari kujionea mapya waliyoyaleta kwenye ulimwengu wa elimu ikiambatana na matumizi ya teknolojia kuwaelimisha wanafunzi mashuleni.
Vyanzo: Gadgets 360, ARS Technica
One Comment
Comments are closed.