Mteja ni mtu anayetakiwa kuheshimiwa daima kwani ndio anayefanya mfanyabiasha apate riziki yake pale anaponunua bidhaa fulani. Wafanyakazi kadhaa wamejikuta matatani huko nchini Australia.
Wafanyakazi kadhaa katika duka la simu la Apple wamefukuzwa kazi kutokana na kukiuka miko ya kazi yao sababu ikiwa ni kuiba picha za wateja na kuzithaminisha kwa kuzipa alama na alama ya juu ikiwa ni 10.
Picha hizo karibu 100 ziliibwa na wafanyakazi hao kutoka kwa wateja hao waliokuwa wameenda dukani hapo kwa ajili ya kufanyiwa matengenezo ya simu yao.
Mpaka sasa Apple imeshafukuza wafanyakazi wanne wakiume kutoka katika duka hilo na Apple wamekataa kukubali kuwa halikuwa kosa la wafanyakazi bali ni wateja wenyewe ndio waliruhusu kitendo hicho kufanyika kwani wafanyakazi wanadai hawakuona kitendo chochote kilichotia shaka kuchukuliwa picha hizo bila idhini ya mtu/watu husika.
Mmoja ya wafanyakazi hao alikuwa akiwapiga picha wadada hao na kisha kuzituma picha hizo kwenye sehenu ya mawasiliano ya wengi na wengine kuanza kuzithaminisha kwa kuzipa alama (rate) huku alama ya juu ikiwa ni 10.
Kila mtu anapaswa kuheshimiwa. Mambo ambayo ni ya mtu binafsi vinatakiwa vithaminiwe. Si kitu kizuri kuchukua kitu fulani bila idhini kutoka kwa mhusika mwenyewe. TeknoKona ingependa kusikia maoni kutoka kwako.
Vyanzo: Telegaph, mitandao mbalimbali