Programu tumishi ambazo zinaelezea kuhusu wanyama zimeonekana kuzorotesha biashara ya utalii na hivyo serikali ya Afrika Kusini yapiga marufuku apps za wanyama.
Applications hizo zimefanya sheria za wanyama kutowekewa mkazo na kufanya ujangiri, rushwa kuongezeka kwa sababu applications hizo zinatoa taarifa kuhusu wanyama mbalimbali ambao taarifa zao zimewekwa katika applications hizo. Mamlaka husika zinataka kuweka katazo kwa applications hizo kutumika kwa sababu ya malalamiko kutoka kwa watu (watalii).
Ni wazi kwamba teknolojia inapanuka siku hadi siku mpaka kufikia kutengeneza app zinazoelezea kuhusu wanyama lakini wangeni (watalii) wanatumia nafasi hiyo vibaya. Vilevile kuwepo kwa apps hizo kuna hatarisha uwepo wanyama mbugani (ujangiri kuzidi kuongezeka).
Inaaminika kuwa utumiaji wa programu tumishi hizo unaleta mkanganyiko kati ya sekta ya utalii na watalii wenyewe kutokana na kuwa yawezekana taarifa ambazo zinakuwa katika apps hizo zinaweza hazijafanyiwa masasisho (updated) ndani ya kipindi kirefu.
Kitendo cha taarifa hizo kutofanyiwa masasisho zinaweza kufanya mtalii kutojua lipi la kushika kutokana na kuwa taarifa zilizo kwenye programu tumishi ni tofauti na anayopata kutoka kwa bwana pori.
Muundaji (developer) wa applications za wanyama alitengeneza programu tumishi ya kwanza ya wanyama akiwa na umri wa miaka 15 na hiyo ilikuwa ni kwa sababu alikuwa ni mpenzi wa kujua maisha ya wanyama mbalimbali (wild life).