Daktari Simon Bramhall mtaalamu wa upasuaji nchini Uingereza amekiri kufanya makosa ya kuweka nembo yake katika maini ya wagonjwa wake aliowafanyia upasuaji.
Daktari huyo mwenye umri wa miaka 53 amekiri kuwa ameacha herufi A na B katika maini ya wagonjwa wake baada ya kuwafanyia upasuaji.
Daktari Simon alifanya makosa hayo katika Hospitali ya Queen Elizabeth huko Brmingham mwezi Februari na Agosti mwaka 2013.
Daktari huyo amekiri mbele ya mahakama kuwa aliandika herufi A na B kwa kutumia mionzi katika maini ya wagongwa wawili aliowafanyia upasuaji mwaka 2013 bila ya ridhaa yao.