Kupitia ukurasa wa Instagram wa #fcbarcatz, Mchezaji wa kimataifa wa uhispania na FC Barcelona Gerard Pique ni miongoni mwa wageni waliohudhuria katika hafla chakula cha jioni kilichoandaliwa na waandaaji wa mkutano mkubwa wa Mobile World Congress (MWC) jijini Barcelona.
Hafla hiyo ya chakula cha jioni ilikuwa ni kwa ajili ya uzinduzi rasmi wa mkutano huo mkubwa wa masuala ya teknolojia duniani.
Mkutano wa MWC wa mwaka huu ulizinduliwa rasmi Jumatatu na hufanyika kila mwaka ambapo huwakutanisha wawakilishi wa makampuni mbalimbali ya simu na kupewa nafasi ya kuelezea matarajio ya kampuni zao.
Mkutano huu huudhuriwa na watu wengi takribani laki moja, aidha vyombo vya habari kutoka kila
upande wa dunia huwepo kufuatailia kinachojiri.
Kupitia mkutano huo taarifa nyingi hutolewa za maendeleo ya simu za kampuni kadhaa, malengo yao na teknolojia mpya wanazotarajia kuziweka sokoni.
Mkutano huo unaochukua wiki moja huanza mwishoni mwa Februari na kuisha mwanzoni mwa Machi kila mwaka katika jiji la Barcelona nchini Uhispania.