Google chrome ilikuwa ndiyo kitumizi cha kwanza kuweza kumjulisha mtumiaji ni tab ipi katika kitumizi chake ambayo ina toa sauti, kumbuka kabla ya hapa ilikua tabu kujua tab ipi kati ya zile ulizozifungua ambayo inatoa sauti (hasa kama umefungua tab zaidi ya moja)
Watengenezaji wengine wa vitumizi wameiga mtindo huo na kwa sasa karibu kila kitumizi kinao huu uwezo wa kukuonesha ni kurasa(tab) ipi ambayo inatoa sauti, shida iliyo baki kwa sasa ni kwamba hauwezi kuwa umefungua kurasa mbili au zaidi kwa wakati mmoja zenye kutoa sauti. Maana zitakuwa zinakuchanganya na utalazimika kusimamisha ukurasa mmoja.
Google chrome imepatiwa uwezo wa kumruhusu mtumiaji kunyamazisha baadhi ya kurasa alizozifungua na kitumizi, uwezo huu sasa utawaruhusu watumiaji kuweza kufungua kurasa zaidi ya moja zinazocheza sauti bila ya usumbufu kwa kuzinyamazisha zile ambazo haziitajiki wakati huo.
Kuanza kutumia utaratibu huu mtumiaji anatakiwa kunakili amri hii chrome://flags/#enable-tab-audio-muting
katika sehemu ya anuani ya kitumizi cha google chrome na kisha kuwezesha (enable) au kukipa uwezo huo wa kunyamazisha. Hii ni namna nyepesi zaidi ya kunyamazisha kurasa zenye sauti bila ya kuzifunga kurasa hizo.
One Comment