Kampuni ya Google imeamua kusitisha uungwaji mkono wa apps za Chrome kwa OS za Linux, Mac na Windows katika kipindi cha miaka miwili ijayo.
Hii inamaana kwamba baada ya miaka miwili basi watumiaji wa kivinjari cha Google Chrome ambao wanatuma apps za Chrome hawataweza kuzitumia tena.
Uungaji mkono unamaana gani?
Tunaposema kusitishwa uungaji mkono hii inamaanishwa kwamba Google hawatajiuhusisha tena na utengenezaji ama kusaidia kutatua matatizo ya app hizo katika OS tajwa pindi itakapofika wakati huo. Hii ina maanisha kwamba itakapofika mwaka 2018 watumiaji wa kivinjari cha Google Chrome katika OS za Linux Mac na Windows hawatakuwa wanatumia app hizi tena.
Kwanini Google wanafanya hivi?
Google wanasema kwamba wanaachana na apps hizi kwa OS tajwa kwasababu matumizi yake yamepungua sana kitu ambacho kimesababishwa na uboreshwaji wa web app hivyo kuzifanya app za Chrome kutokuwa na umuhimu sana.
Nini kitatokea kwa watumiaji wa Google Chrome?!
Kwa watumiaji wa Google Chrome hata hivyo wataendelea kuzipata na kuzitumia app hizi kwa kuwa Google wanasema kwama app za Chrome ni muhimu kwa ufanyaji kazi wa kivinjari cha Chrome. Na pia watumiaji wa kompyuta zinazotumia programu endeshaji ya Chrome OS, yaani Chromebooks, wataendelea kupata apps hizo bila tatizo lolote.
Vyanzo: mtandao wa Gadgets360 pamoja na mitandao mingine ya Teknolojia