Kampuni ya Simu ya Huawei ya nchini Uchina imekuwa ya pili kwa mauzo ya simu duniani yaliyofanyika katika kipindi cha robo ya tatu ya mwaka huu na kuipiku kampuni ya simu ya Marekani, Apple.
Kwa muda mrefu Kampuni ya Huawei imekuwa nafasi ya tatu ya uuzaji wa simu nyingi duniani nyuma ya vinara Samsung na Apple kwa muda wa miaka saba.
Katika robo ya tatu kwa mwaka 2018 Samsung imeweza kuuza simu 71.9m sawa na 20% ya soko, Huawei wakiweza kuuza simu janja 54.2m ikiwa ni sawa na 15% ya soko lote na Apple wakiwa wameuza simu takribani 41.3m ambapo ni sawa na 12% ya soko lote.
Kwa mujibu wa ripoti hiyo Huawei imeweza kutawala soko la simu kwa robo ya pili ni baada ya kutoa simu mpya ya Huawei P20 Pro yenye vidokezo pekee ambavyo hakuna kwa simu zilizoko sokoni. Simu hiyo ya Huawei P20 Pro inayoelezwa kusaidia ukuaji huo iliingizwa sokoni Machi 2018.