Tecno ni kampuni kubwa sana katika kutengeneza na kuuza simu, mara zote simu zake zimekua ni mkombozi mkubwa kwani unapata kitu kizuri kwa gharama ndogo.
Baada ya fununu nyingi kuvuja kuwa Tecno wanakuja na simu janja kali kwa kushirikiana na klabu kubwa ya mpira wa miguu duniani ijulikanayo kama Manchester City, kifaa kimeingia sokoni
Kusoma Kuhusu Fununu Hiyo Ingia Hapa
Toleo la simu jipya kutoka tecno (Tecno Camon CX Toleo la Man City) litakua linapatikana kwa muda fulani tuu. Hili litakua ni toleo la kupita kulingana na jinsi muungano wa pande mbili hizo ulivyo
SIFA ZAKE ZA NDANI
KAMERA :
- Kamera ya mbele inapiga picha kali kwani ina MP 16, Pia ina uwezo mkubwa wa kupiga picha katika mwanga mdogo kwani ina flashi mbili kwa pale mbele ambazo zitakusaidia kupata ‘selfie’ kali.
- Kamera ya nyuma (pia MP 16) inapiga picha kwa uharaka zaidi. Hii inachukua sekunde 0.1 moja tuu kupiga picha kwa kutumia alama za vidole (finger print).
- Uwezo wa kurekodi video
PROSESA :
- 1.5GHz Octa Core Processor
KIOO :
- 5.5 FHD IPS display
RAM :
- GB 4
UjAZO :
- Ujazo wa uhifadhi wa ndani ni GB 64.
- Unaweza ukaongezea ujazo wa nje (Memori kadi) kama ukipenda
NETWORK :
- Insapoti mpaka teknolojia ya 4G yenye kiwango cha juu.
BETRI :
- Uwezo wa betri ni 3200 mAh
OS :
- Program endeshaji ni Android 7.0 Nougat ikiwa na HiOS
SIFA ZINGINE:
- Uwezo wa alama za vidole (fingerprint)
- Uwezo wa kujaza chaji kwa haraka (“Light Speed” Charging)
Simu hii inapatikana katika maduka yote ambayo yanauza vifaa halali vya kampuni ya Tecno au kwa maulizo zaidi ingia hapa