Moja ya kampuni nguli kabisa katika utengenezaji magari mbalimbali – Volvo kufungua kiwanda nchini Kenya.
Kampuni hiyo imepanga kuwekeza Shilingi bilioni 2.5 za Kenya ambazo ni takribani Sh. Bilioni 52 – 54 za Kitanzania na hivyo kufanikisha utengenezaji wa haraka wa kiwanda hicho kwa ajili ya utambulisho rasmi kufikia mwezi Machi mwaka 2018.
Kiwanda hichi kitakuwa ni cha tatu barani Afrika kwa kampuni ya Volvo, tayari wana viwanda vingine nchini Afrika Kusini na Morocco. Wanategemea katika kipindi cha mwaka mmoja waweze kuzalisha magari 500, baadae wanataka kukuza uzalishaji huu na kufikia magari 2000 kwa mwaka.
Kiwanda hicho kitatengenezwa kwa ubia na kampuni nyingine ya Kenya ambayo imekuwa ni muagizaji pekee wa magari ya Volvo kwa soko la Afrika Mashariki, ya NECST Motors.
Ajira takribani 300 za moja kwa moja zinategemewa kutengenezwa na kiwanda hicho.
Lengo kuu kwa Volvo ni kuhakikisha wanazidi kukua na kushikilia vizuri soko la magari la Afrika Mashariki. Wanafanikio ya kushikiria soko la magari aina ya maroli/mabasi kwa asilimia 20 nchini Morocco na asilimia 18 nchini Afrika Kusini na sasa lengo lao ni kufikia asilimia 20 pia Afrika Mashariki.
Volvo ni kiwanda cha nne cha utengenezaji magari nchini Kenya. Kiwanda cha Volkswagen kiliacha utengenezaji takribani miaka 40 iliyopita ila nacho kimeanza utengenezaji magari nchini humo tena. Pia tayari makampuni mengine kama vile Peugeot, Iveco na Ashok Leyland wameshatangaza nia za kufungua viwanda nchini humo pia.