Kijana mmoja nchini Norway alijikuta akiwa amenasa na kushindwa kutoka kwenye choo baada ya kuingia ili kuchukua simu iliyokuwa imedondokea chooni.
Rafiki yake kijana huyo inasemekana alidondosha simu yake kwenye shimo la choo wakati anakojoa. Ni choo cha kadamnasi (public toilet), kijana huyo akajitolea kwenda kuitoa simu hiyo.
Inasemekana kijana huyo aliingia kwenye choo cha mfumo wa tenki chini ambacho huwa kinatolewa uchafu mara kadhaa tuu kwa mwaka.Ā
Inasemekana kwa akili yake alifikiri kitakuwa hakina uchafu mwingi kwa wakati huo ila alipoingia ndani akajikuta amesimama kwenye uchafu uliomfikia hadi maeneo ya mapajani. Alitapika, akashindwa kuipata simu na baada ya hapo ndio alianza kuangaika kutoka.
Alipojaribu kupanda tena kupitia tundu la choo alilotumia alinasa, na hivyo kushindwa kutoka hadi pale watu jiji walipokuja kumtoa.
Mara moja baada ya kutolewa alipelekwa hospitali alipooga na kuchomwa sindano za kuzuia maambukizi.