Tovuti za habari nchini Tanzania na ulimwenguni kote zimekuwa chanzo cha habari katika ulimwengu wa teknolojia na kufakia watu kiurahisi zaidi kupitia vifaa mbalimbali vya kidijitali.
Katika ulimwengu wa teknolojia blog/tovuti ina sehemu kubwa katika kuwafikia wale ambao unawalenga kitu hucho kifike kwao lakini ulishawahi kujiuliza kinachofanyika ili kuifanya tovuti (blog) kuwa hewani?
Gharama kadha wa kadha huwa zinalipwa na mojawapo ni leseni ya biashara, jina la tovuti, upatikanaji wake kwenye intaneti, n.k. Katika siku za hivi karibuni imeelezwa kuwa sasa wamiliki wote wa blog itabidi walipe kiasi cha pesa zitakazoingia serikalini.
Ili kuidhinisha kama mtoa habari kwa njia ya mtandao mwombaji ibidi ajaze fomu kuweka makadirio ya kiasi cha fedha alichowekeza, idadi ya wakurugezi, wanahisa, kiasi cha hisa wanazomiliki, viwango vya elimu vya wafanyakazi wao, tarehe wanayotarajia kuanza kazi na bila kusahau mpango mkakati wa ukuaji wa biashara yao.
Kwanza mamlaka husika itahakiki watoa habari wote kwa njia ya tovuti (bloggers) kisha kutakiwa kulipa kiasi cha $930|Tsh. 2,092,500 kwa mwaka ili kutambulika na kupewa leseni.
Hata baada ya blog kuidhinisha kufanya kazi zake bado mamlaka husika itakuwa na nguvu ya kuamuru makala fulani iondolewe kama inaonekana inaleta uchochezi, kuhatarisha usalama wa nchi, inachukiza na kuamuru makala husika kuondolewa ndani ya saa 12 vinginevyo kulipa faini ya $2,210 au kwenda jela mwaka mmoja.
Hata wale wanaotoa matangazo ya redio, televisheni kwa njia ya intaneti nao tozo ya $930 kila mwaka itawahusu na huenda ikaathiri upatikanaji wa habari.
Kama unfikiria kuanzisha blog yako basi haya ni machache tu ambayo inabidi uanze kuyafikiria namna ambayo utayaweka sawa na kila kitu chako kuhusu utoaji wa habari kwa njia ya mtandao kiende sawa.
Vyanzo: Quartz Africa, iAfrikan