Baraza la Ushauri la Watumiaji wa Huduma za Mawasiliano ni chombo kilichoundwa kisheria chini ya Kifungu cha 37 cha Sheria ya Mamlaka ya Mawasiliano Na. 12 ya mwaka 2003 kwa madhumuni ya kulinda na kutetea maslahi na haki za mtumiaji wa huduma na bidhaa za mawasiliano Tanzania katika nyanja za Teknolojia ya Habari na Mawasiliano, Utangazaji, Posta, Vifurushi na Vipeto.
Baraza hili lina majukumu yafuatayo:
1. Kuwakilisha maslahi ya watumiaji wa huduma za mawasiliano zinazosimamiwa kisheria kwa kushauriana na Mamlaka, Waziri mwenye dhamana ya mawasiliano, na mawaziri wa sekta.
2. Kupokea na kusambaza taarifa na maoni kuhusu masuala ya msingi ya watumiaji wa huduma za mawasiliano.
3. Kuanzisha kamati za watumiaji katika ngazi za mikoa, wilaya na sekta na kushauriana na kamati hizo.
4. Kufanya mashauriano na wahusika katika sekta, serikali na makundi mengine ya watumiaji wa huduma kuhusiana na masuala ya msingi ya watumiaji wa huduma zinazosimamiwa kisheria.
5. Kutumia zaidi vipindi vya Radio na Luninga kusudi Baraza lisikike na kukusanya maoni ya Wananchi
6. Kukusanya na kuwasilisha maoni ya Wananchi kwa vyombo husika
7. Kuandaa ,utaratibu na mbinu za kuhamasisha jamii kwa kuanzisha Kamati za Watumiaji wa huduma katika ngazi za Mkoa na Sekta.
8. Kutembelea na kujifunza mbinu za kuelimisha na kuwasilisha maoni ya wateja kutoka nchi zilizopiga hatua kubwa katika maeneo haya (showcases).
9. Kutayarisha semina, kongamano, washa na wadau na kutoa maazimio ya pamoja.
10. Kuhudhuria kongamano na Semina za Kimataifa ili kujifunza mwelekeo wa dunia wa Taarifa ya Habari ya Mawasiliano pamoja na kujadili masuala muhimu ya watumiaji.
11. Kufanya utafiti wa kina na masuala ya msingi ya watumiaji (Customer Satisfaction Survey). Kutumia mtandao wa TOVUTI na Barua Pepe ili wateja wa huduma za mawasiliano watoe mawazo yao wapate taarifa za uhakika hususani maendeleo na mabadiiiko katika sekta hii muhimu.
12. Kujenga nguvu ya pamoja na Mabaraza mengine ili kuweza kushinikiza watumiaji wa huduma za serikali ili mlengwa apate huduma za viwango vya juu, zenye ubora na kwa bei nafuu kabisa. Kubuni mikakati mbadala na endelevu inayolenga kutatua matatizo ya watumiaji katika sekta ya mawasiliano.
13. Kufanya tathmini za mara kwa mara ya mikakati ya kutetea haki za wateja.
Kwa maelezo zaidi kuhusiana na TCRA-CCC tembelea tovuti yao hapa.
No Comment! Be the first one.