Katika dunia ya leo ambayo ipo kidijitali zaidi kuna njia mbalimbali za mtu kuweza kufika mahali mpaka ulipo na hii inatokana na kipengele muhimu sana kwenye Google ambacho kinasaidia kitu fulani kionekane kwenye ramani.
Si haba unaweza ukawa unamiliki biashara ambayo inafahamika na wengi kutokana na kwamba umeitangaza kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii kitu ambacho sio kibaya kabisa lakini itakuaje kwa yule ambae hafahamu biashara yako ilipo? Hapo ndipo linapokuja suala zima la kuifanya mahali ilipo ofisi ifikike kirahisi hata kwa yule anayetumia mwongozo wa Dira.
Unaweza kuwa umeona kwenye tovuti mbalimbali zikionyesha mahali ambapo ofisi husika ilipo basi tambua ya kuwa kuna hatua zilifuatwa mpaka eneo husika likaweza kuonekana kwenye ramani:
Hatua ya kwaza: tembelea maps.google.com kisha wengiza anwani ya eneo/mtaa ambapo ofisi yako ipo kisha bofya “Enter“.
Hatua ya pili ni kurekebisha/kujaza (bofya palipoandikwa suggest edits>>change name or other details) taarifa kamili za ofisi/biashara husika. Hapa ndipo utakapotakiwa kujaza jina la kampuni /biashara, anwani ya mtaa, saa za kazi, namba ya simu, tovuti (ambayo ipo hewani tayari), n.k.
Hatua ya tatu ni kusambaza kwa watu. Hii itasaidia kuwafahamisha wateja ni wapi ilipo biashara yako na kuweza kufika bila shida yoyote/kusumbuka ukitafuta ofisi ilipo.