Tume ya TEHAMA ya Tanzania imeandaa kongamano la pili ambalo linajulikana kama “Annual ICT Professionals Conference 2018” ikiwa ni moja kati ya juhudi zake katika kukuza tehema tanzania.
AIPC ni moja kati ya majukwaa muhimu sana kwa wana TEHAMA wote kwani ni sehemu ambayo unaweza ukapata mambo kede kede ikiwemo kama vile kujua jinsi maswala ya TEHAMA yanavyokwenda duniani, kutengeneza mahusiano na watu mbalimbali katika kongamano hata kuonyesha bidhaa zako (kama unazo) n.k.
Ijulikane kwamba kongamano hilo kwa mara ya kwanza lilifanyika mwaka jana katika ukumbi wa mikutano wa mwalimu nyerere, japo na mwaka huu litafanyika huko huko mambo mengi makubwa yanategemewa kutoka katika kongamano hili.
Kongamano linaweza hudhuriwa na mtu yeyote lakini inapidi alipie ushiriki wake, hivyo kwa maelezo zaidi juu ya kujiandikisha unaweza kutembelea: www.ictc.go.tz : au barua pepe: info@ictc.go.tz
Ikumbukwe kwamba kongamano hili linaweza kuhudhuriwa kwa kujiandikisha tuu na si vinginevyo. TeknoKona ni moja kati ya mbia/mshirika katika AIPC 2018.
Kongamano litakua ni la siku tatu na litaanza tarehe 24 mpaka 26 mwezi Oktoba 2018. Mada mbalimbali zitazungumzwa ikiwemo na maudhui ya nyumbani kuhusiana na TEHAMA, ubunifu na ujasiliriamali. Ukuaji wa viwanda na hata ulinzi na usalama haswa ule wa mtandaoni.
Mambo kama changamoto za kuanzisha kitu (Biashara) katika TEHAMA tanzania yatazungumzwa, pia kutakuwa na maonyesho kutoka kwa wawekezaji na pia hata uwekezaji utakuwepo katika nyanya mbali mbali za TEHAMA.