Apple bado inaendelea kuwa kwenye vichwa vya habari kutokana na bidhaa zake zilizozinduliwa mapema mwezi Sept. 2018 kuonekana kuwa si shwari.
Yapo mengi sana yanayozungumzwa kuhusiana na simu rununu ambazo Apple walizitambulishwa kwa ulimwengu Sept. 12 lakini sasa baadhi ya iPhone XS na XS Max zimebainishwa na waliozinunua kuwa na shida upande wa kuchaji.
Tatizo lenywe ni kutokubali kuchaji iwapo haitoi mwanga (kioo kinakuwa kimezima); tatizo hilo ni kwenye kimemeshi cha iPhone XS na XS Max.
Ili kuweza kufanya simu hizo kuchaji basi inabidi zinawaka (mwanga ukionekana kwenye kioo) kisha kuchomoa na kuchoka tena kimemeshi.
Apple wamekuwa kimya kuzungumzia suala hilo ingawa upande wa teknolojia ya kuchaji bila kutumia waya hauna shida.
Vyanzo: Engadget, Forbes