Katika moja ya kifaa cha michezo ya kujifurahisha zaidi ya miongo miwili iliyopita huweza kukosa kutaja Game Boy kutokana na kwamba kutokea kupendwa na wengi wetu tulitumia kucheza magemu.
Miaka imepita na teknolojia imekua, tangu mwaka 1998 ambapo ndio ilitolewa kwa mara ya kwanza Nintendo kampuni inayojihusisha na utengenezaji wa magemu inatarajia kuirudisha tena kifaa hicho lakini katika utofauti.
Siku si nyingi zilizopita Nintendo walienda kuainisha mchoro wa mfuko wa simu kwa nia kuumiliki (patent) ulionyosha mfuko wa simu unaofanana na “Game Boy“.
Bidhaa hiyo mbali na kulinda simu isidhurike inapodondoka lakini kila kitufe kikibonyezwa kitaleta majibu kama vile kwenye kioo cha mguso.
Bidhaa hiyo haitakuwa inaingiliana kwenye simu zote hivyo Nintendo watatengeneza mifuko tofauti tofauti kulingana na simu husika.
Vyanzo: Extreme Tech, Hype Beast