Teknolojia katika matibabu nchini inazidi kukua ambapo Ssrikali imezindua huduma za uchunguzi binafsi wa ugonjwa wa kifua kikuu (TB).
Uzinduzi wa huduma ya kifua kikuu kupitia teknolojia ya simu za mkononi unaojulikana kama “TAMBUA TB” umezinduliwa Septemba 21 na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Mhe. Dkt. Faustine Ngugulile.
Huduma hiyo inayopatikana kwa njia ya simu bila malipo itampasa mtumiaji wa simu kupiga namba *152*05# BILA MALIPO ilikuweza kupata menyu ya “Afya na Ustawi wa Jamii” na kisha utabonyeza nambari sita (6) kufika kwenye kipengele kinachihusu kifua kikuu.
Itakubidi ufuate kila hatua na ujibu maswali kwa usahihi. Baada ya maswali kukamilika mfumo huo utakupa majibu kama una dalili za ugojwa wa kifua kikuu au la!
Iwapo mteja atagundulika hana TB atashauriwa kujiunga na ujumbe mfupi wa simu wenye kutoa elimu ya kifua kikuu na aliyegunduliwa atasajiliwa kwenye mfumo wa mtoa huduma za afya.
Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile amesema Wizara yake itawezesha ufanisi na ufuatiliaji wa mfumo huo na kuhakikisha taarifa zinakusanywa na kutumika ipasavyo.