Miaka 10 ya iPhone. Kampuni ya Apple imetangaza kwamba imeuza simu zake za mkononi za iPhone bilioni 1.2 tangu kuanza kwa uzalishaji wa simu hizo mwaka 2007.
Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Mtandaji bwana Tim Cook jumatano wiki katika mkutano wa kutangaza mapato ya robo ya tatu ya mauzo yake kwa miaka 10.
Mwaka jana Apple walitangaza kuuza simu zao zipatazo bilioni 1 hivyo inamaana kwa mwaka mmoja wameuza simu zipatazo milioni 200. Simu janja ya Iphone (1st generation) zilizinduliwa kwa mara ya kwanza Juni 2007 na Steve Jobs.
Cook amesema mauzo ya Iphone yamepanda hasa kwa simu ya Iphone 7 Plus baada ya kuzidi mauzo ya Iphone 6s kulinganisha na robo ya juni mwaka jana. Iphone 7 iliuzwa mara mbili yake.
Mbali na maadhimisho hayo ya miaka 10 ya Iphone, mashabiki wa simu janja wanasubiri kwa hamu kuzinduliwa rasmi kwa simu ya Iphone 8.