Moja kati ya bidhaa zinazofanya vizuri sokoni kutoka kwa kampuni nguli ni AirPods ambazo zinaonekana kusambaa (kununuliwa) hivyo watu wengi kuwa nazo lakini pengine wateja wa Apple na ulimwengu kwa ujumla wakafurahi zaidi!.
Naamini utakuwa unafahamu vyema ule mkebe wa kutunza zile AirPods ambazo zinavutia kweli kweli hasa kwa jinsi zilivyoundwa na kutoona hata chembe ya waya isipokuwa zenyewe tu ambazo ni ndogo na kamwe hazichoshi kuwa nazo popote pale.
Kwa taarifa zilzosambaa kwenye tovuti mbalimbali inaaminika kuwa Apple wapo kwenye mpango wa kuwezesha mikebe ya kutunza AirPods kuwa na uwezo wa kuchaji iPhone 8, 8+ au X.
Teknolojia inayozungumziwa hapa na kuwa uti wa mgongo katika kufanikisha suala hilo ni kuchaji simu janja bila kutumia chaji ya waya nikiwa na maana kuchaji simu kwa teknolojia ya bila waya ambapo iPhone 8 na kuendelea ina uwezo huo.
Teknolojia hii huenda ikaanza kuonekana kwenye mikebe ijayo ya AirPods itakayotolewa mwezi Septemba kama ilivyo desturi ya Apple kutoa simu mpya (iPhone) pamoja na bidhaa nyingine mwezi huo.
Hakuna uhakika sana kuhusu mikebe hiyo ya kuhifadhia kutoka mwezi Septemba 2018 lakini inaaminika kuwa iwapo teknolojia hiyo ikiongezwa itawasaidia Apple kuuza AirPods zaidi ya 28 milioni.
Vyanzo: Engadget, 9to5mac
One Comment
Comments are closed.