Miaka kadhaa baada ya kuacha masomo chuo kabla ya kuhitimu na kuamua kujikita katika ujenzi wa Facebook. Mark Zuckerberg, Mwazilishi wa Facebook apata shahada.
Zaidi ya Muongo mmoja ulipita aliamua kuacha chuo na kwenda kuanzisha mtandao maarufu sana duniani ulio na watumiaji wa kila siku wanakaribia bil. 2 – Facebook.
Facebook ilianzishwa mwaka 2004 na Bw. Mark Zuckerberg pamoja na mwanzilishi mweza ambao wote walikuwa ni wanafunzi wa chuo cha Harvard. Bofya –>Historia ya Facebook. Hivi karibuni katika chuo kile kile ambacho Bw. Mark Zuckerberg aliachia masomo yake ametunukiwa shahada ya heshima (honorary degree) katika fani tofauti na ile aliyokuwa akiisomea zaidi ya muongo mmoja uliopita.
Mark Zuckerberg ambaye ni mtu wa tano tajiri duniani, ulio na thamani ya dola za kimarekani bilioni 62.3, amerudi katika chuo kikuu cha Harvard kutoa hotuba ya kuhitimu na kupokea shahada ya staha.
Soma pia: Historia ya Facebook
Katika sehemu ya hotuba yake Zuckerberg aliwaambia wahitimu kwamba tunaishi katika wakati ambao haujaimarika. Hizi ndio jitihada za wakati wetu, nguvu za uhuru, uwazi na jamii duniani dhidi ya nguvu za utawala wa kimabavu, kutengana na utaifa.
Mmoja wa wageni katika mahafali hayo alikuwa mkewe Bw. Mark na alinyoosha kidole kuelekea katika bweni alilokuwa akikaa (mumewe) wakati alipouzindua mtandao wa Facebook, na kutaja kwamba kukutana naye katika sehemu hiyo, ilikuwa ndio kitu bora alichopitia akiwa chuo kikuu.
Katika hitimisho katika hotuba yake aliwaambia wanaafunzi wasiunde “nafasi za ajira tu, bali wawe na malengo”. Sisi ndio TeknoKona, tupe maoni yako sasa.
Chanzo: BBC