Kampuni ya utengenezaji kompyuta kwa ajili ya matumizi ya uchezaji magemu, Razer, watambulisha laptop yenye vioo vitatu (display) kwa wakati mmoja.
Laptop hiyo ambayo kwa sisi inafahamika kwa jina la kimatengenezo zaidi, Project Valerie, imetambulishwa kwenye maonesho ya bidhaa za elektroniki huko jijini Las Vegas nchini Marekani.
Laptop hii inakuwa ya kwanza duniani kuja na mfumo huu.
Kikawaida inaonekana kama laptop ya kawaida ila kwenye kioo kioo kikuu vingine viwili vinavyochomoka upande wa kulia na kushoto na kujipanga.
Kilaa screen/display/kioo kimoja kina ukubwa wa inchi 17, takribani sentimenta 43. Display zake ni za kiwango cha juu cha HD, 4K.
Uwepo wa screen tatu kunaweza mfanya mtu afikiri laptop hiyo itakuwa nene sana pale itakapofunikwa, ila wamejitahidi kuifanya isiwe nene sana. Ina unene wa inchi 1.5, takribani sentimita 3.81.
Kampuni ya Razer bado hawajatoa muda rasmi ambao laptop hizo zitaingia sokoni ila lazima bei yake itakuwa juu kidogo ila inategemewa kwa wapenzi wa magemu ambao tayari wamezoea kutumia display zaidi ya moja katika uchezaji wa magemu kwenye kompyuta watakuwa tayari kujitoa na kununua laptop hii.