Safaricom yapigwa faini. Kampuni ya mawasiliano ya simu Safaricom nchini Kenya, imetozwa faini ya mamilioni ya fedha kwa sababu ya huduma mbovu.
Kampuni hiyo ilitozwa KSh. 270.1 milioni|Tsh. 7,290,000,000 na Mamlaka ya Kusimamia Mawasiliano nchini humo (CAK) katika kipindi cha mwaka uliokamilika mwezi Machi 2017.
Mwaka jana, kampuni hiyo ilitozwa faini ya Sh. 157 milioni. Katika ripoti iliyozinduliwa mwishoni mwa wiki jana; kiwango hicho ni asilimia 0.15 ya mapato yote ya kampuni hiyo kabla ya kutozwa ushuru, Machi 2017.
Kampuni hiyo ilifuata kanuni kufikia asilimia 62.5, kiwango kilicho chini ya kiwango kilichopendekezwa cha asilimia 80. Safaricom iliimarika katika viwango vya utoaji huduma kutoka asilimia 50 mwaka jana, ongezeko la asilimia 12.5.
Baadhi ya masuala yanayozingatiwa na CAK kutokuwa na uwezo wa kumaliza mazungumzo kwa wateja na ubora wa sauti.