Simu ya Samsung Galaxy S8 baada ya kupitia majaribio kadhaa imeonekana ndio simu ambayo ni rahisi zaidi kuvunjika kuliko simu zingine zozote kwa sasa.
Kutokana na aina ya ubunifu wa kioo/display kwenye simu za Samsung Galaxy S8 na S8 Plus kumeifanya simu hizo kuwa rahisi zaidi kuvunjika kuliko simu zingine zozote.
‘Simu moja ya Galaxy S8/S8 Plus ikianguka mara moja tuu chini ina asilimia kubwa zaidi kuvunjika kioo chake vibaya ukilinganisha na simu zingine’
Utafiti ulijumuisha simu hizo kuangushwa kutoka urefu wa futi 6 na kuangukia kwenye eneo la sakafu. Kampuni moja wapo, SquareTrade, ambayo huwa inafanya tafiti za namna hii kwa simu za aina mbalimbali imesema simu za S8 ndio simu za kwanza kwenye utafiti wao kuvunjika maeneo mengi zaidi kwa kuanguka mara moja tuu.
Habari nzuri?
Habari nzuri ni kwamba Samsung wamehakikisha vipuri (spare) za simu hizi zitakuwa bei rahisi zaidi ukilinganisha na matoleo ya simu za familio hiyo zilizopita – screen/kioo chake kitakuwa bei nafuu zaidi kwa tofauti ya bei ya kati ya tsh 100,000 hadi 200,000 ukilinganisha na cha Galaxy S7.
Pia Samsung wamekuja na vijikava vidogo kwa ajili ya kuvalisha simu hizo. Ukivalisha kikava hichi basi athari ya kuanguka na kuharibiba vibaya inapungua zaidi ukilinganisha na kama ikianguka bila kava hii.
Kava hizi zitauzwa kwa takribani Tsh 40,000/= na zitaweza tumika kwenye simu za aina zote za S8.
Ulipitwa na uchambuzi wa simu ya Samsung Galaxy S8 na S8 Plus? Soma hapa – Uchambuzi, Samsung Galaxy S8 na S8 Plus
Chanzo: Mitandao