Samsung wapo kazini kuja na aina ya monitor iliyo pana zaidi na yenye lengo la kuondoa ulazima wa watu kutumia mfumo wa kuunganisha monitor mbili au zaidi.
Utumiaji wa kompyuta unaohusisha uhitaji wa kuunganisha monitor zaidi ya moja ni maarufu zaidi kwa wacheza magemu, maofisini.
Monitor hii inaupana wa inchi 49 na inakuja kwa kiwango kikubwa tuu cha ubora wa mtazamo – Double Full HD (Resolution ya 3840×1080).
Pia itakuwa imepinda kidogo (curved) ili kumsaidia mtazamaji kuona kwa ubora mzuri zaidi.
Samsung wameshawekeza katika teknolojia ya utengenezaji wa monitor hizi kwa wingi zaidi. Utengenezaji mkuu unatarajiwa kuanza kufanyika mwezi wa tisa na hivyo hadi kufikia mwakani katikati basi monitor hizi zinaweza anza kuingia sokoni.
Bei yake bado haijawekwa wazi ila mara nyingi monitor huwa zinapatikana kwa bei nafuu zaidi ukilinganisha na bei za luninga (TV).
Chanzo: TheNextWeb