Kulingana na tovuti ya Forbes inasemekana kampuni ya Samsung imehakikisha imechukua oda zote za prosesa ya kisasa zaidi ya Snapdragon 835 zinazotengenezwa na kampuni ya Qualcomm kiasi ya kwamba washindani wake itabidi watumie prosesa za matoleo yaliyopita kwenye simu zao mpya.
Prosesa ya Snapdragon 835 ni moja ya prosesa ya kisasa zaidi kwa sasa na simu nyingi za kisasa zinazokuja kutoka makampuni mengine mengi nguli zilitegemewa zitumie prosesa hizo – ila kutokana na Samsung kuweka oda kubwa ina maanisha wengine kama vile LG na HTC waliokuwa na lengo la kuweka prosesa hiyo kwenye simu zao kisasa kutumia prosesa toleo la nyuma (Snapdragon 821).
Simu ya Samsung Galaxy S8 inategemewa kutambulishwa rasmi mwezi wa nne mwaka huu nchini Korea Kusini. Utumiaji wa prosesa hii ya kisasa utaifanya simu ya Samsung Galaxy S8 kuwa moja ya simu zenye kasi kubwa zaidi sokoni.
Qualcomm ni moja ya kampuni nguli katika utengenezaji wa malighafi (‘parts’) mbalimbali muhimu zinazotumika kwenye vifaa vya elektroniki kama vile simu janja na kompyuta.
Simu za familia ya Galaxy S ni moja ya matoleo ya simu yanayoletea Samsung mapato makubwa sana katika biashara ya simu janja – ukujumlisha pia na simu za familia ya Galaxy Note.