Samsung ni moja ya kampuni ambayo kamwe imekuwa haisemi ni simu gani ya kampuni yake itakuwa inapata toleo jipya la Android pale toleo hilo linapokuwa tayari kwa simu za mfumo wa Android.
Hata hivyo watumiaji wa simu za Samsung hupokea toleo jipya miaka miwili au zaidi pale toleo jipya linapokuwa tayari. Hii inachangiwa na kampuni hiyo kufanya marekebisho kadhaa kwa toleo jipya la Android ili liendane sawia na simu zake kwa kuweka apps zake ndani yake.
Toleo jipya la Android Oreo limekuwa likisubiriwa kwa muda mrefu na watumiaji wengi wa simu za Samsung lakini wamekuwa hawana uhakika ni simu gani ndio zitakazopata au kukosa toleo hilo.
Kuna taarifa za uvujaji zilizotolewa za majina ya simu za Samsung ambazo zitapata toleo la Oreo. Matoleo ya Samsung Galaxy S8 na S9 yameanza kupata toleo la Oreo Beta.
Watumiaji wa simu za Samsung Galaxy watasubiri mwanzoni mwa mwaka 2018 kuanza kupata toleo la Oreo. Hata hivyo orodha hii haijathibitishwa bado na wenyewe Samsung.
Katika orodha iliyotolewa simu za Samsung Galaxy A7 (18), Samsung Galaxy A5 (18) na Galaxy A3 (18) hizi bado hazijazinduliwa rasmi na zinatarajiwa kuzinduliwa mapema mwaka 2018 na zitakuwa na Android Nougat lakini baada ya muda mfupi zitapata masahihisho na kupata toleo la Oreo.
Ifuatayo ni orodha ya simu za Samsung galaxy zitakazopata toleo la Oreo:-
Galaxy S series
Galaxy S8 na S8 Plus
Galaxy S7 na S7 edge
Galaxy S6 na S6 edge
Galaxy S6 edge Plus
Galaxy Note series
Galaxy Note8
Galaxy Note7 (FE)
Galaxy Note5
Galaxy A series
Galaxy A7 (18)
Galaxy A5 (18)
Galaxy A3 (18)
Galaxy A7 (17)
Galaxy A5 (17)
Galaxy A3 (17)
Galaxy A9 pro (16)
Galaxy A8 (16)
Galaxy J series
Galaxy J7 (2016)
Galaxy J7 pro
Galaxy J5 pro
Galaxy J7+
Galaxy J7 max
Galaxy J7 prime
Galaxy J7 core
Galaxy C series
Galaxy C10
Galaxy C9 pro
Galaxy C7 pro
Galaxy C5 pro
Galaxy C7
Galaxy Tab series
Galaxy Tab S3
Galaxy Tab S2
Galaxy Tab A (17)
Galaxy Tab A (16)
Galaxy Tab active 2